166.Wamwendea Yesu
1. Wamwendea Yesu
kwa kusafishwa,
na kuoshwa
kwa damu ya Kondoo?
Je neema yake
umemwagiwa?
Umeoshwa
kwa damu ya Kondoo?
Kuoshwa, kwa damu
itutakasayo ya Kondoo;
Ziwe safi nguo nyeupe
mno:
Umeoshwa
kwa damu ya Kondoo?
2. Wamwandama daima
Mkombozi na kuoshwa
kwa damu ya Kondoo?
Je, waishi kwake
msulibiwa?
Umeoshwa
kwa damu ya Kondoo?
Kuoshwa..
3. Atapokuja Bwana arusi
uwe safi kwa damu ya
kondoo.
Yafae kwenda Mbinguni
mavazi
yafuliwe
kwa damu ya kondoo.
Kuoshwa….
4. Yatupwe yaliyo na
takataka,
na uoshwe kwa damu ya
Kondoo
Huoni kijito chatiririka
na uoshwe kwa damu ya
Kondoo?
Kuoshwa….
Comments
Post a Comment