164.Tumekujia Bwana Wetu
1. Tumekujia Bwana wetu
kujiweka mkononi
mwako,
tuwe wako, hata milele
twakushukuru na
twakusifu.
Mwokozi wetu, utukubali,
utuongoze njia ya mbingu.
2. Twataka kubatizwa leo
kwa Jina lako, tuwe
Wakristo.
Umetukomboa na sisi
ulipokufa pale Golgota,
na kwamba wewe upo
karibu,
unasikia kuomba kwetu.
3. Twakupambia mioyo leo,
ingia, Mfalme wa utukufu!
Utupe sisi nuru yako
tuwe mwanga katika
dunia.
Pokea leo mioyo yetu,
tunajitoa kwako wenyewe.
4. Tunakuomba sasa, Bwana,
usitutie majaribuni.
Utuongoze siku zote,
tukufuate wenye imani.
Mwisho tufike kwenye enzi
kuu, tuipokee taji ya
mbingu.
Comments
Post a Comment