163.Mungu Upokee Moyo Wangu

1. Mungu upokee 
moyo wangu wote, 
niwe mtoto wako, 
siku zangu zote.
Nikufuate Wewe 
nisikuache tena, 
nishike siku zote, 
ulivyotuagiza.
Unisaidie mimi,  
hata kufa kwangu.


2. Msalabani pako,
Yesu naanguka, 
uliyenifia 
hata mimi pia.
Yaondoe makosa 
yatoweke kabisa, 
nipate kuwa safi 
kwa damu yako bora.
Unisaidie mimi
Hata kufa kwangu.


3. Roho Mtakatifu, 
   unanipa nguvu, 
  niweze kushinda 
  majaribu yote,
  naomba: utawale
  kataika moyo wangu,
  Shetani, hata kufa, 
  asinishinde mimi.
 Unisaidie mimi,
 hata kufa kwangu.


4. Baba, Mwana, na Roho 
uliye mmoja tu, 
niliye maskini 
nakuomba sana: 
Unikubali sasa, 
katika ubatizo, 
futa makosa yangu 
kwa maji haya bora.
Unisaidie mimi, 
hata kufa kwangu.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu