162.Bwana Twakuletea
1. Bwana, twakuletea
mtoto huyu,(watu hawa)
tukijua
amri yako ya mwisho
uliyowapa mitume:
Watu wote wabatizwe,
watakao kuwa wako.
2. Neno hili ni kubwa
tulilopewa na Yesu:
Atakaye kufika
katika ufalme wako,
hana budi kuzaliwa
tena kwa maji na Roho.
3. Pokea kondoo wako
Mchunga mwema Bwana
Yesu
Umwongoze mbinguni
(Waongoze mbinguni)
ndiwe njia na uzima.
Umpe kukutegemea
(wape kukutegemea)
apate kukutengamana
(wapate kutengemana).
4. Baba, tunakusihi
ukubali wimbo wetu,
usikie maombi
tunayokuomba sasa.
Andika jina la mtoto
(Andika majina yao)
katika kitabu chako!
Comments
Post a Comment