162.Bwana Twakuletea

1. Bwana, twakuletea 
mtoto huyu,(watu hawa) 
tukijua 
amri yako ya mwisho 
uliyowapa mitume:
Watu wote wabatizwe, 
watakao kuwa wako.


2. Neno hili ni kubwa 
   tulilopewa na Yesu:
  Atakaye kufika 
   katika ufalme wako, 
  hana budi kuzaliwa 
   tena kwa maji na Roho.


3. Pokea kondoo wako
Mchunga mwema Bwana
Yesu
Umwongoze mbinguni
(Waongoze mbinguni) 
ndiwe njia na uzima.
Umpe kukutegemea
 (wape kukutegemea) 
apate kukutengamana
 (wapate kutengemana).


4. Baba, tunakusihi 
ukubali wimbo wetu, 
usikie maombi 
tunayokuomba sasa.
Andika jina la mtoto
(Andika majina yao) 
katika kitabu chako!



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu