159.Mbinguni, Mbinguni

1. Mbinguni, mbinguni
Kuna mji mwema.
    /:Wapendeza sana, 
       ni wake Mungu,:/


2. Milango ya mjini 
 ni dhahabu tu,
/: mungu ndiye jua 
anaung`aza.:/


3. Ugonjwa hauko,
 kufa hakuna.
   /:Wenyeji wa humo 
     ni wa kweli tu:./


4. Waimba usiku 
hata na mchana
/: Wakimsifu Bwana 
  Mungu wetu tu.:/


5. Wote waimbao
 wana furaha.
/:Wang`azwa na damu 
ya Bwana Yesu.:/


6. Vijana sikieni 
wote kwamba.
  /:Twapendwa na Yesu,
  Bwana wa mbingu.:/


7. Twendeni kuingia 
wote mjini,
/:Tupewe uzima 
na Bwana wetu!:/



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu