154.Ninataka Kuingia

1. Ninataka kuingia 
mjini kwa Mungu.
Nitashinda, nitakaza 
mwendo nifike, 
nikishikwa na shida, 
nikichoka njiani,
Yesu unaniambia:
“Uningojee!”


2. Naitwa na Yesu Kristo 
enzini mwake. 
Nakimbia, kukawia 
hakuna faida,
 wote wachelewao 
hawapati taji.
Mimi sitaki kingine 
ila uzima.


3. Elekeza macho yangu 
mlangoni pako.
Niongoze, nipe nguvu, 
ninapochoka.
Ninapojaribiwa, 
ninaposingiziwa,
Yesu, unisaidie 
Nisikuache.


4. Mkono wako unishike 
nisianguke.
Najiona kuwa mnyonge,
 nguvu i kwako,
Neno lako, ee Yesu,
 linanipa uzima.
Nikifika, nitaimba,
“Umeniponya!”



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu