151.Ee moyo Wangu Hima

1. Ee Moyo wangu, hima, 
enenda mbinguni!
Ulimwenguni humu 
hapana raha.
Mchungaji wetu Yesu 
achungapo kondoo 
ni penye raha kuu.
Enenda mbinguni!


2. Yeye akupokee,
Mungu Baba yako, 
akuketishe pake 
katika enzi kuu.
Atakuvika nguo 
za wongofu wa Mungu, 
akupa raha kuu.
Enenda mbinguni!


3. Nakutamani sana
Mwana Kondoo Mungu!
Ningepata mabawa 
ningeruka pale, 
wanaposhangilia 
malaika wake Mungu 
katika raha kuu.
Enenda mbinguni!


4. Mapenzi yako Bwana 
ndizo haja zangu,
Utakalo lolote 
nami nitatenda.
Naingojea siku 
utakayoniita, 
nipate raha kuu!
Enenda mbinguni!



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu