148.Mungu Baba Mungu Mwana
1. W:Mungu Baba, Mungu
Mwana,
Mungu Roho, twakusifu
twakushangilia sote,
umejifunua kwetu
kwa upendo,
kwamba wanadamu
wakujue wote.
K:/:Mungu wetu
W:Anapenda tuwe
Wake
K: Dhambi zetu
W:Tuache, tumfuate.:/
2. W: Mungu Baba wewe
uliumba vyote,
Mbingu, dunia
navilivyomo vyote,
watu ndege na
wanyama uliumba, Jua
mwezi na nyota
vyakutukuza.
K:/: Mungu wetu:/
3. W: Mungu Mwana,
wewe ulikuja kwetu,
ukaishi kama
mwanadamu kweli,
ukateswa na kubeba
dhambi zetu,
kwamba sisi tupate
wokovu kweli.
K:/: Mungu Wetu:/
4. W: Mungu Roho,
uliye kiungo chetu,
wakusanya
na kuita watu wote,
tufundishe kumjua
Bwana wetu,
na utukufu wake
hata milele.
K:/: Mungu wetu:/
Comments
Post a Comment