95.Bwana Yesu Alikufa


1. Bwana Yesu alikufa
 kwa sababu yetu sisi,
 alipata duniani
 maumivu mengi sana.


2. Bustanini akiomba
 akafadhaika kabisa.
 Jasho lake kama damu
 nchini ikadondoka.


3. Wayuda wakamwendea,
 wakamshika,
 wakamfunga.
 Na rafiki zake wote
 wakimbia, wakamwacha.


4. Na wale wakampeleka
 barazani kumhukumu.
 Wamhukumu yule
 mfalme,
 atakayewahukumu.


5. Wakamfyoza, wakampiga,
 wakampeleka Golgota.
 Pale wakamwamba mtini,
 kwa misumari kumkaza.


6. Kukawa na giza huko,
 nchi ikatetemeka.
 Watu walioko wote,
 Wakaona woga mwingi.


7. Na saa tisa ikifika,
 Yesu apaza sauti kuu,
 kwamba: Yamemalizika;
 mara akakata roho.


8. Askari wakamwendea,
 wakamwona amekufa.
 Nao wakamchoma mkuki;
 ukapenya moyo wake.


9. Damu yake ikatoka,
 yakatoka maji tena.
 Maji, damu iwezayo
 kuosha uchafu wote.


10. Na watu wema
 wamshusha,
 wamfunga katika sanda,
 wakamweka kaburini,
 na penye mlango jiwe
 kuu


11. Siku ya tatu atoka
 Yesu Kristo kuzimuni,
 alivyotanganza kwanza.
 Yu mzima hata milele!.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu