92.Ukiwa na Vichache
1. Ukiwa na vichache
Umtolee Bwana,
kwani akiba yako
ataiongeza.
Vipaji vyako haba.
Yeye hakatai,
kidogo kwako wewe,
kwake kitazidi!
2. Vile vile na moyo
umtolee Bwana!
Ndivyo vipaji vyema
vinavyompendeza.
Kwani sisi wenyewe,
alitukomboa,
akiuawa Yeye
kwa kuwambwa mtini.
3. Ukiwa na ubaya
umwambie Bwana!
Ukishandana nao,
atakutakasa.
Damu aliyotoa,
ndiyo itoshayo,
kuosha wakosaji,
hata wewe hivyo.
4. Vitu vya mali nyingi
umtolee Bwana!
Alitoka mbinguni
kusumbuka hapa.
Alikufa mwenyewe
kwa ajili yako,
nawe hutoi chako
kwa ajili yake?
5. Wakristo na tutoe
shukrani kwa Mungu.
Hiyo ndiyo shukrani
ya wokovu wetu.
Injili yake Kristo,
ienee pote!
Kwa ushuhuda wetu
watu waokoke.
Comments
Post a Comment