88.Nataka kusimama


1. Nataka kusimama 
chini ya msalaba, 
kama kivuli cha mwamba
wakati wa mchana, 
kama ni maji nyikani, 
kambi safarini, 
na hapa nitapumzika, 
kwani jua kali.


2. Mahali pema sana 
chini ya msalaba, 
kwani hapo ninaona 
upendo wa Yesu.
Yakobo alivyoona 
ndotoni zamani, 
mti Yesu aliowambwa, 
ni ngazi kwa Mungu.


3. Juu ya msalaba huo
Yesu alikufa
Alikufa tuokoke.
Tuliopotea.
Ninastaajabu kabisa 
ni mambo mawili:
Kwake Yesu ni upendo,
Kwangu mimi kosa!


4. Wataka kuonana 
na Yesu mbinguni, y
akupasa kukaa kwanza 
chini ya mti huo.
Ni kweli siku chache tu 
mateso na shaka.
Halafu pasipo mwisho 
furaha kwa Bwana! 



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu