84.Nimshangilie Bwana Wangu

1. Nimshangilie 
Bwana wangu 
na kumwimbia
Mkombozi,
katukomboa msalabani,
nisifu pendo lake kuu.
    Haya mwimbieni Yesu,
    amekubali mateso
    katukomboa
    msalabani,
    tusifu pendo lake kuu!


2. Tumsifu Yeye 
Mponya wetu
 katika ulimwengu huu, 
katupatanisha na Baba
tulio wakosaji tu.
      Haya mwimbieni...


3. Katuletea mwanga wake, 
   tulikaa katika giza, 
   wokovu ukaonekana, 
  kamshinda mwovu, 
  ni shujaa!
       Haya mwimbieni….


4. Na tumtukuze Bwana 
    wetu,
    tumtumikie kwa bidii,
   na atawale apendavyo,
    na sisi sote tuta mtii!
    Haya mwimbieni……



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu