83.Yesu Kuteswa Kwako

1. Yesu kuteswa kwako 
nitakufikiri.
Nipe kwa shauri hili
roho na mbaraka.
Moyo wangu uone 
hali yako Yesu,
jinsi ulivyoteswa 
kwaajili yetu.


2. Moyo wangu uone 
taabu yako kubwa, 
maumivu, mapigo, 
na kuwambwa mtini,
 taji lako la miiba 
tena misumari, 
iliyokuumiza, 
hata kufa kwako.


3. Nikitazama yote 
yaliyokutesa, 
nikifikiri sababu 
na maana yake.
Sababu ndio mimi 
na makosa yangu: 
umepata mateso, 
nipate huruma.


4. Yesu unifundishe 
nijute kwa moyo;   
nisikuzidishie 
shida na uchungu.
Nisiweze kupenda 
yaliyokutesa:
nataka kuyaacha 
na kukufuata.




Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu