81.Ulimwengu tazama
1. Ulimwengu Tazama,
Yesu mwokozi wako
asulubiwavyo.
Mwenye heshima Yote
anayavumilia
mateso tena matusi.
2. Karibia tazma
maungo yake yote
yatokavyo damu.
Na moyo wake mwema
kwa shida na uchungu
unaugua vigumu.
3. Nani akupigaye,
aliyekufanyia
mambo kama haya?
Wewe huna makosa
kama wengine wote,
hujui kosa lolote.
4. Makosa yangu mimi
yaliyo kama mchanga,
hayahesabiki, ndiyo yakutiayo
mateso na chungu
uliyoyavumilia.
5. Mimi nimestahili
kulipa haya yote,
na kufungwa sana.
Mapigo na mateso
uliyoyapata wewe
yalitoka kwangu mimi.
6. Umejitwika mzigo
ulio mzito sana
kuliko jiwe kuu.
Wachukua maovu,
Tupate kuokoka
tukae nawe daima!
Comments
Post a Comment