79.Nakusalimu Kichwa


1. Nakusalimu kichwa
Kilichojaa damu,
Kilichovikwa taji
La miiba mikubwa,
Kilichopata enzi
Kwa Mungu mbinguni,
Kitukanwacho sasa
Matusi makali.


2. Naona uso wako 
watemewa mate, 
heshima yako yote 
imeondolewa.
Mwanga wa macho yako
wazimika sasa.
Aliyekuharibu  
hivi, ndiye nani?


3. Mateso yako Bwana,
Yanipasa mimi.
Wewe waadhibishwa
Kwaajili yangu.
Hukumu unapata
Iliyonipasa.
Bwanangu nakuomba,
Unihurumie!


4. Na mimi na simama 
msalabani pako;
niwe karibu kwako
utoapo roho;
ukiugua sana 
kwa teso la kufa, 
nitakushika Bwana
kwa moyo wa upendo.


5. Bwana nayashukuru 
masumbuko yako, 
sababu ya kuteswa 
na kufa kuchungu.
Wewe umenishika, 
nami nakushika, 
mwisho nitakufia
 uliyenifia.


6. Moyo unaposhikwa
 na woga wa kufa, 
usiniache Bwana
 katika vita hii.
Siku ya kufa kwangu
 unisaidie, 
kufa kwako kuchungu 
kutaniokoa.


7. Niwie kama ngao 
nitakapokufa, 
nione uso wako
katika uchungu.
Ndipo nikukumbatie!
Anayekufa hivi
afa kwa amani.



Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu