78.Mwokozi Wangu Umekosa Nini?

1. Mwokozi wangu 
umekosa nini? 
Wahukumiwa kama mwuaji.
Umeshtakiwa makosa
Mangapi uliyotenda?


2. wapigwa sana 
 miiba taji lako,
umetemewa 
mate,
watukanwa, 
wanyweshwa nyongo 
tena siki kali.


3. Sababu gani 
unateswa hivi?
Makosa yangu yanakuumiza;
 mateso haya yako yanipasa, 
mimi mkosaji.


4. Ajabu kubwa 
sana tendo lako;
mchungaji unateswa kwa
ajili ya kondoo,
Bwana 
unawalipia watumwa wako.


5. Tuliopokuwa mateka
wa mwovu, 
nawe ukaja ukatukomboa.
Tulistahili kufa kwa
Milele,
Ukatufia.


6. Mwokozi wangu 
nifanyaje mimi, 
niitangaze pote sifa yako?
Nakufuata nikutumikie
 maisha yote.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu