56.Mmoja ni Mfalme

1. Mmoja ni mfalme shujaa,
Ni mshindaji!
Enyi adui, kimbieni tu!
Nawe sayuni uone furaha
ukapumzishe kabisa 
moyo:
Uzima, utengamano,
furaha ndizo Mwokozi
atakazokupa.


2. Twende kuonja
maji ya uzima
tunayopewa
na Bwana Yesu
aliyesema
“Njooni kwangu nyote”
nitapumzisha mioyo
yenu.”
Nyweni, wapenzi,
katika kisima
chenye wokovu
wa wenye huzuni.


3. Mfalme wa mbingu
akuwapa
kilemba kizuri cha 
urembo,
awawekea vitu vya milele,
heshima hiyo ni ya 
kushinda.
Vumilieni taabu na shida:
Yesu mwenyewe
ni tuzo la vita.


4. Nguvu, ujuzi,
heshima na sifa
ni zake Mungu
na Mwana Wake.
Nami nataka kufika 
mbinguni!
Nifunguliwe mafungo
yangu!
Mwenye upendo atanisikia.
Wenye uzima wanamsifu
Mungu.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu