54.Yesu u Nyota Kubwa


1. Yesu, u nyota kubwa,
itokayo kwa Yakobo,
Moyo wangu wapenda
kukutumikia leo.
Ukubali vipaji 
niviletavyo mimi.


2. Ninaleta dhahabu,
            Ndio kukutegemea,
            Nalo ni paji lako,
            Ulilonipa mwenyewe;
            Nikushike kwa kweli
            Hata majaribuni.


3. Nao uvumba wangu
              ni maombi yangu mimi,
              midomo na mioyo
             Usikome kuyatoa.
             uyakubali haya
             kuwa uvumba mzuri.


4. Nayo majuto yangu
Ndiyo manemane yako;
Kwani hunipokea,
Nikikujutia kweli.
Nasema kwa furaha:
Watwaa matunzo yangu!



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu