51.Yesu ndiye kiongozi wangu
1. Yesu ndiye kiongozi
wangu,
kumfuata Yeye ni furaha,
ajuaye kuongoza vema,
anilinda nisione shida,
analeta raha moyoni.
2. Bwana Yesu akiniongoza,
Nitapita pori na misitu,
Nitavuka mito na bahari
Kwa furaha, kwani nina
njia
ya kufika mjini kwa Mungu.
3. Nikilala Yesu anilinda
anitunza Yeye siku zote.
Hata nikifika njia panda,
Nikiona shaka, aonyesha
njia ya kufika kwake.
4. Siku zote namfuata Yeye,
Sitaona kiu wala njaa;
anitunza kwa rehema
nyingi:
nitaweka mikononi mwake
moyo wangu, auokoe.
Comments
Post a Comment