47.Anza Siku Yako Hii


1. Anza siku yako hii
     kwa jina la Yesu;
     Mwombe akujalie,
     usimame naye.
     Kazi zako zote wee
     atazibariki.
     Na tena ulalapo,
     atakuwa kwako.


2. Asubuhi mapema
Umwombe Mwokozi,
akusaidie Yee
shidani popote.
Atasimama kwako
Siku kuchwa pia,
na kumshinda
Shetani akikujaribu.


3. Yesu akiwa nawe,
waacha maadui,
usiogope hila
zao zote mbaya.
       Umtegemee Yesu,
shika mkono wake;
mtegemee Mwokozi,
Yeye atashinda.


4. Mambo yangu na shida
          ninakuwekea
          kama unavyopenda,
          zimalize zote.
          Kazi yangu nianze
          kwa jina la Yesu
          nakuomba: njoo kwangu,
         unisaidie!



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu