139.Mungu Atukuzwe pekee

1. Mungu atukuzwe pekee, 
   shukrani zitolewe 
   sababu ya rehema kuu 
   aliyotutendea. 
    Mungu atupenda sana, 
    sababu hii ametupa 
     kutengemana vema.


2. Twakutukuza Baba mkuu 
     twakuheshimu sana, 
     sababu ya kutawala 
       zamani hata leo. 
      Nguvu zako haziishi 
      utakayo yatendeka, 
      Muumba wetu ndiwe.


3. Twakutukuza ee Yesu
   Mwana wa Mungu wetu,
   Uliyetupatanisha 
   na Baba mwenye enzi.
 Mwana Kondoo wa 
 Mungu, 
 sikia tukikuomba
 Mwokozi wetu ndiwe.


4. Twakutukuza ee Roho 
uliyekuja kwetu.
Uwape nguvu Wakristo 
waliokombolewa.
Utuokoe shidani.
Shetani asitushinde,
Mtuliza mioyo ndiwe.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu