129.Twaomba Roho wa Mungu

1. Twaomba:Roho wa Mungu
Mfariji wetu mkuu,
Utupe baraka.
Yesu alipotuaga,
Kasema: Namtuma 
Roho wangu kwenu.


2. Utuamshe wakosaji 
    kwa kuwa tu kondoo 
    waliopotea.
    Uokoe ulimwengu, 
    umeharibika, 
    upate kujuta.


3. Roho wa ujuzi mwingi, 
   fundisha Wakristo 
   wampendeze Mungu.
   Utufundishe kuomba 
    kwa Mungu vizuri, 
     tusikiwe naye.


4. Utusaidie sana, 
   tumshinde shetani 
   na dunia pia.
   Tusitengwe na Mwokozi, 
   yakija mateso, 
   shida na huzuni.


5. Twakuomba uwe nasi 
   tulio wanyonge 
   tukijaribiwa.
   Mwisho tuakapokufa, 
   tuone furaha 
   baada ya mateso.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu