128.Roho Mtakatifu Uje


1. Roho Mtakatifu uje 
 utukalie na sisi, 
 fanya makao kwetu. 
  Utupe nuru ya mbingu, 
  ung’aze mioyo yetu, 
  tumtumikie Mungu.
 Uje, lete utukufu 
 na furaha na uzima, 
  haya twafuata kwako.


2. U chem chem yenye rehema, 
   unatunywesha hekima, 
   watufundisha vema, 
    tujue kuwaambia 
    wenzetu wasiojua 
    habari za wokovu.
     Roho zetu uzifanye, 
      tuyatende mambo mema 
      wewe utukuzwe sana.


3. Umande mzuri 
  wa mbingu 
   geuza mioyo yetu, 
   tujae pendo lako.
   Tupendane na wenzetu, 
    tuwafanyie mema tu 
    na kweli watu wote.
    Kwetu uwe upendano,
     kugombana kuwe mbali, 
     tuwe na amani daima


4. Ututakase mioyo, 
   utupe nguvu rohoni, 
  ushike mwendo 
  mwema.
 Tusifuate kiburi, 
 tamaa mbaya za mwilini 
 na mambo ya duniani.
Roho zetu ziongozwe 
zifikiri mambo yako, 
mpaka tufikapo kwako.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu