127.Karibu Kwangu Roho

1. Karibu kwangu Roho 
  ingia moyoni, 
  uliyeniletea 
   uzima na raha.
   Roho Mtakatifu 
   wa Baba na wa Mwana 
   ufananaye nao 
   ukaaye nao.


2. Unafundisha watu 
   kuomba vizuri, 
   wapate kusikiwa 
   na Mungu mbinguni.
   Unatuombea, 
   hukomi, mpaka Mungu 
   atende mambo yale 
   uliyoyaomba.


3. Wafurahisha moyo, 
  hupendi huzuni, 
  tukiwa matesoni, 
  unatutuliza.
  Wazungumza nasi 
   kwa Neno lako tamu, 
   unatia mioyo 
   furaha ya kweli.


4. Unatufanya sisi 
   kuwa usharika, 
  hutaki tugombane 
  na kuchukiana.
  Wanaopigana 
  unawapatanisha, 
  wataka wapendane
  Wakristo wowote.


5. Ulinde nchi yetu, 
  serikali yetu, 
  tukae na amani 
 duniani humu. 
 Uwape wakubwa, 
 pamoja na wadogo 
uchaji na akili, 
 wampendeze Mungu.


6. Katika mwendo wetu 
   utupe na sisi 
   nguvu, tumshinde mwovu 
   akitujaribu.
   Utusaidie, 
   tushike njia yako 
   na mwisho tufe vema 
   tufike kwa Mungu.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu