125.Tazameni Anapaa

1. Tazameni, napaa, 
  mwenye kushinda vita, 
  gari lake ni mawingu, 
  ndipo anapopita, 
   malaika wa mbinguni 
   wakimwimbia Bwana,
  Amekaribishwa sasa, 
   kwa kufurahi sana.


2. Ni nani anayepaa, 
   wote wakimsifu?
  Ndiye Bwana mwenye 
  enzi, 
  ndiye Mungu wa Safu, 
    aliyeteseka kwanza 
    mle katika mti, 
    kwa kifo chake 
    mwenyewe,
    akashinda mauti.


3. Akaaga watu wake, 
   na akawabariki 
  akapaa mawinguni 
   na wakimwangalia,
  chini hutenda ya Mungu, 
   yote yakitimia, 
   kazi yake imekwisha, 
    kwake amerejea.


4. Ni kuhani wetu sasa,
   yumo na damu yake, 
   katika patakatifu 
  twapatanishwa kwake,
  Amefanya ukombozi 
   kuondoa dhambi zetu,
  Mungu amekubali 
  ndiye sadaka yetu.


5. Mwili ameuinua 
   huo wa ki-Adamu, 
  ndani yake sisi sote 
  pia tuna sehemu 
  Mungu na Mtu pamoja 
  yuko huko enzini 
  twaamini Bwana, 
  kwamba 
   tutakwenda mbimguni.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu