122.Shujaa Mkubwa

1. Shujaa mkubwa,
Bwana wetu,
leo umejikalisha
kitini kwa Babako.
Ufalme wote ni wako,
umeshinda maadui,
hawana nguvu tena.
Umepewa enzi kubwa,
kufa pia na uzima,
vyote unavitawala.


2. Malaika wote
wa mbingu
wanakusifu kwa nyimbo
wanakutumikia.
Ulipotoka mbinguni
ukaja kutuokoa,
na umerudi leo.
Sasa, wako utukufu;
nasi tunakushukuru,
tunasifu Jina lako.


3. Twataka kutafuta tu
ufalme wako wa mbingu.
Utupe nguvu zako,
tushike mwenendo 
mwema,
tusiwe wenye kiburi
ila wanyenyekevu.
Tuepuke kila kosa,
tufuate njia yako
ya kuingia mbinguni.


4. Yesu mwana wa Daudi
uliyetupatanisha
na Bwana Mungu wetu.
Ulipokwenda mbinguni
umetutengenezea
makao ya milele.
Tuongoze, tusichoke,
tusafiri siku zote;
kwani watungoja kwako.



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu