113.Bwana Yesu Kafufuka
1. K: Bwana Yesu kafufuka,
ametoka kaburini.
W: Haleluya, Haleluya,
ametoka kaburini
2. K. Na mashaka yalizuka,
hapakuwa tumaini,
W:Haleluya, Haleluya,
ametoka Kaburini
3. K: Wanawake walifika
asubuhi kaburini.
W:Haleluya, Haleluya,
ametoka Kaburini
4. K: Tayarini waliweka
manukato mkononi.
W: Haleluya, Haleluya,
ametoka Kaburini
5. K: Walitaka kuupaka
mwili mle kaburini
W:Haleluya, Haleluya,
ametoka Kaburini
6. K: Nao hao walifika;
Kumbe jiwe li kandoni.
W: Haleluya, Haleluya,
ametoka kaburini
7. K: Kwa ukweli malaika
kasimama kaburini.
W: Haleluya, Haleluya,
ametoka kaburini.
8. K: Wakasema kafufuka;
enyi nyote kumbukeni.
W:Haleluya, Haleluya,
ametoka kaburini.
9. K:Wanawake wakumbuka;
watoka kaburini
W:Haleluya, haleluya
ametoka Kaburini.
10. K: Kweli Yesu kafufuka,
ametupa matumaini.
W:Haleluya, Haleluya,
ametoka Kaburini
11. K:Atazidi kwa neema
kuokoa waamini.
W: Haleluya, Haleluya,
ametoka Kaburini
Comments
Post a Comment