113.Bwana Yesu Kafufuka

1. K: Bwana Yesu kafufuka, 
ametoka kaburini.
W: Haleluya, Haleluya, 
ametoka kaburini


2. K. Na mashaka yalizuka, 
hapakuwa tumaini,
W:Haleluya, Haleluya,
ametoka Kaburini


3. K: Wanawake walifika 
   asubuhi kaburini.
  W:Haleluya, Haleluya,
  ametoka Kaburini


4. K: Tayarini waliweka  
    manukato mkononi.
W: Haleluya, Haleluya, 
     ametoka Kaburini


5. K: Walitaka kuupaka 
    mwili mle kaburini
W:Haleluya, Haleluya, 
   ametoka Kaburini


6. K: Nao hao walifika;
        Kumbe jiwe li kandoni.
  W: Haleluya, Haleluya, 
         ametoka kaburini


7. K: Kwa ukweli malaika
       kasimama kaburini.
W: Haleluya, Haleluya, 
      ametoka kaburini.


8. K: Wakasema kafufuka; 
       enyi nyote kumbukeni.
W:Haleluya, Haleluya, 
     ametoka kaburini.


9. K:Wanawake wakumbuka;  
      watoka kaburini
W:Haleluya, haleluya 
      ametoka Kaburini.


10. K: Kweli Yesu kafufuka, 
          ametupa matumaini.
     W:Haleluya, Haleluya, 
         ametoka Kaburini


11. K:Atazidi kwa neema 
          kuokoa waamini.
     W: Haleluya, Haleluya, 
           ametoka Kaburini



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu