112.Leo Siku ya Furaha
1. Leo siku ya furaha,
Kila mtu ashangilie,
Kristo Yesu afufuka,
ateka adui wote!
Haleluya!
2. Nyoka wa kale na kifo,
Kuzimu hata ubaya
Vimeshindwa
na mshindaji
Yesu Kristo Mfalme
wetu!
Haleluya!
3. Mateka yote ya kifo
yamekamatwa na Yesu,
na ufu umenyang’anywa
naye aliyefufuka!
Haleluya!
4. Adui hawatushiki
tunakwenda uzimani,
tunapokunywa naye
kinywaji kipya milele!
Haleluya!
5. Jua na mwezi na nchi,
Viumbe vyote vya Mungu
Vinafurahiwa leo:
Mfalme wa uongo
ashindwa!
Haleluya!
6. Kwa hivi tushangilie,
tumwimbie Yesu Kristo,
Yeye ametuokoa,
afufuka kaburini!
Haleluya!
Comments
Post a Comment