104.Yesu Amefufuka
1. Yesu Amefufuka,
sitakuogopa kufa.
Amefufuka, naye
atanifufua mimi.
Atanipa mwili mpya:
ni tumaini langu.
2. Yesu amefufuka,
anapatawala pote.
Nami nitatawala
pamoja naye milele.
Atimiza agano:
ni tumaini langu.
3. Yesu amefufuka,
yanipasa kumngojea.
Mwenye kumtegemea
Bwana wetu, ataona
rehema yake Mungu:
Ni tumaini langu.
4. Yesu amefufuka,
naweza kumtumikia,
na shindana na tama,
moyo wangu uwe safi
Atanisaidia:
Ni tumaini langu.
5. Yesu amefufuka,
siwezi kutengwa tena
na Yesu Bwana wangu.
Kwa mateso au furaha.
Vyote havinishindi:
Ni tumaini langu!
6. Yesu amefufuka,
ni mlango wa kuingia
furahani mbinguni.
Nitatulizwa nikifa,
nikiweza kusema:
U tumaini langu!
Comments
Post a Comment