103.Moyo Yafurahie Yafanywayo

1. Moyo yafurahie, 
    yafanywayo leo:
   Mwanga umetokea 
gizani mwa kufa.
Mwokozi kalazwa, 
tutakapozikwa, 
roho ikiisha 
kurudi mbinguni.


2. Alipozikwa Yeye 
adui acheka.
Lakini akashindwa:
Kristo afufuka.
Atokea shujaa
 bendera mkononi, 
kwani ameteka 
mateka ya mwovu.


3. Ni jambo kubwa 
   hili lenye furaha kuu.
Sitaogopa sasa 
uchungu wa kufa, 
 na yote mengine 
 yatakayoteka  
 mali nipewayo 
 na Yesu Mwokozi.


4. Namshika siku zote
Mwokozi wangu mkuu.
Yeye ni kichwa chetu 
sisi tu viungo.
Dunia makosa
Shetani na kufa
Yeye kawashinda, 
nami namfuata.


5. Afika furahani 
nami nitafika,
Sitaona huzuni
Na shida zozote.
Mkubwa wangu Yesu 
ataniakingia 
vinavyonidhuru,
Yeye ngao yangu.


6. Nitakapoingia 
mbinguni, naona 
andiko la furaha
Linasomwa hivi:
Ashindaye kule
Aingia hapa, 
anayejidhili 
atakuzwa hapa!



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu