102.Haleluya Tumwimbie


1. Haleluya! Tumwimbie 
   tumsifu sana Bwana wetu,
   tumshangalie kwa shangwe,
  akafungwa na adui 
  alipokufa msalabani,
  lakini sas yu hai.
  Habari njema hii:
  Mesiya anakaa mzima kweli.
  Haleluya! Tumsifuni!
  Tumsifuni Mungu wetu.


2. Haleluya! Tumwimbie, 
tumsifu sana Bwana wetu, 
tumshangilie kwa shangwe
Watu wana shida sana, 
taabu nyingi na huzuni 
mpaka watakapokufa.
Furaha yetu hii:
Bwana ametoka kaburini.
Haleluya! Tumsifuni!
Tumsifuni Mungu wetu!


3. Haleluya! Tumwimbie 
tumsifu sana Bwana wetu, 
tumshangilie kwa 
shangwe.
Atatufufua sisi, 
tutafika rahani kwake, 
tuishi pamoja naye.
Tumwamini Yeye 
Mwokozi wetu mkuu, 
mwenye nguvu.
Haleluya! Tumsifuni!
Tumsifuni Mungu wetu!



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu