100.Mungu Tusaidie


1. Mungu tusaidie, 
   sisi tunaangamia.
    Nchi imeharibiwa 
    na mwovu wake Shetani
   Kweli kweli ndiye Yesu 
   aliyewambwa mtini 
    penye mlima wa 
   Golgotha 
    aokoe wenye dhambi.


2. Kaonyesha huruma,
  Wayuda wakasumbua.
  Wakampiga makofi,
  Pilato aliamua.
      Kweli kweli ndiye Yesu…


3. Yesu mwenye upendo
   alikubali kuuawa, 
   damu ilimwagika 
   ili sisi tuokoke.
        Kweli kweli ndiye Yesu…..


4. Pale msalabani,
Bwana Yesu aliteswa 
mzigo wa dhambi zetu, 
ulimwangukia yeye, 
Kweli kweli ndiye Yesu…..


5. Sote na tukumbuke, 
kifo cha Mwokozi wetu.
Alisema ya kwamba 
jililieni wenyewe.
    Kweli kweli ndiye Yesu.


6. Habari zilisemwa,
    Mahali hapa hayupo, 
    ona alipokuwa, 
    jiwe limeondolewa. 
    Kweli kweli ndiye Yesu…


7. Ni ajabu kabisa 
   wingu kuja kumpokea.
   Habari ilisema 
   Yesu atarudi tena.
       Kweli kweli ndiye Yesu….



 

Comments

Popular posts from this blog

17. Tuimbe na kusifu

32 Kitoto Mpenzi Lala Wee

143.Mungu ni wa Utukufu