152.Mahali pa Raha

1. Mahali pa raha
 ya moyo wapi?
Akukingiaye 
mabaya nani?
Dunia haina makimbilio, 
nisiposhindwa 
na makosa yangu.
   /: Sipo sipo hapa sipo 
      mbinguni ni ngome 
       ya moyo wangu.:/


2. Iache dunia, 
uone ngome, 
unapofurahishwa
 moyo wangu.
Ni Yerusalemu 
unaojengwa 
na mawe mazuri 
ya dhahabu tu.
     /:Ndiko, ndiko, 
     ndiko ngome 
     na makimbilio 
      ya moyo wangu.:/


3. Mwangani kwa Yesu 
  ni raha tamu, 
hakuna makosa 
na shida huko.
Vinubi na sauti 
za nyimbo nzuri 
zinaufurahisha moyo
 huko.
  /:Raha, raha, raha 
     tamu
    mbinguni kwa Yesu 
     naitamani.:/



 

Comments