91.Ni damu Idondokayo

1. Ni damu idondokayo 
mwilini mwa Yesu, 
wakosaji wakioga, 
husafishwa kweli
   Bwana wangu.
 Mungu wangu,
 U uzima wangu, 
 umekutana na kufa 
 kwa ajili yangu!


2. Ilimpatia wokovu 
mwizi kule mtini, 
nami nisiyemtafuta, 
inanisafisha.
 Bwana wangu….


3. Shaushi aliyemlinda
Yesu akiteswa, 
naye akamshuhudia: 
ni mwana wa Mungu!
Bwana wangu….


4. Nipe ulimi mpya Yesu 
   wa kukuimbia, 
  Babayo tutamtukuza
 Jina lake pekee.
   Bwana wangu….. 



 

Comments