91.Ni damu Idondokayo
1. Ni damu idondokayo
mwilini mwa Yesu,
wakosaji wakioga,
husafishwa kweli
Bwana wangu.
Mungu wangu,
U uzima wangu,
umekutana na kufa
kwa ajili yangu!
2. Ilimpatia wokovu
mwizi kule mtini,
nami nisiyemtafuta,
inanisafisha.
Bwana wangu….
3. Shaushi aliyemlinda
Yesu akiteswa,
naye akamshuhudia:
ni mwana wa Mungu!
Bwana wangu….
4. Nipe ulimi mpya Yesu
wa kukuimbia,
Babayo tutamtukuza
Jina lake pekee.
Bwana wangu…..
Comments
Post a Comment