80.Liko Neno Moja Nipendalo

1. Liko Neno moja nipendalo,
ni chakula cha moyo,
Neno hili linanituliza 
nikipatwa na shida:
Kumtazama Bwana Wetu 
pale, 
atoapo jasho kama damu,
akubalipo mzigo,
Baba aliomtwika


2. Siku zote 
namkumbuka yeye,
 alivyosulubishwa, 
akivumilia taabu kimya 
kama mwana wa kondoo.
Nami akanikumbuka 
mimi,
akisema: Yamemalizika!
Huko aliniteka, 
nami niwe mtu wake.


3. Bwana wangu, 
u mwenye huruma,
 mimi ni mkosaji tu; 
nilipokuwapo penye giza
 wewe ukatokea, 
ukamtafuta kondoo wako,
 kabla mimi sijakusikia.
Watoa ukombozi 
unipao uhuru.



4. Ndimi huru lako,
Bwana Yesu, 
wewe ndiwe Bwanaangu.
Jina lako, bora liung’aze
moyo wangu vizuri.
Amani yako nikae nayo,
Siku zangu zote mpaka
 kufa.
Ndivyo ninavyoomba,
Bwana unikubali.



 

Comments