140.Tumsifu Sisi Watu


1. Tumsifu sisi watu, 
  tumsifu Mungu Baba, 
   aliyeumba vyote 
   kwa nguvu yake kuu.
  Wazima watu wote, 
   na ndege wa angani 
   wanyama wa mwituni, 
     kwa huruma yake.


2. Tumsifu sisi watu, 
   tumsifu Bwana Yesu, 
   aliyetukomboa 
   kwa damu yake tu.
   Amani tumepewa, 
   hatuna hofu tena
   Ametuhurumia,
   Mwokozi ni yeye.


3. Tumsifu sisi watu, 
   tumsifu Roho, ndiye 
   mtulizaji popote, 
    furaha iwe kuu.
    Moyo umetulia, 
    amani umepata.
   Awatakasa wote, 
    wamwombao yeye.



 

Comments